Sunday, 25 August 2013

 KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPYA TANZANIA 2013.
 N i wazi kuwa kira raia wa Tanzania na asiye wa Tanzania anjua kuwa  Tanzania imeungana na nchi nyingine katika mabadiliko ya katiba. mataifa mengi ya afrika na amerika kusinii na caribian zimekuwa katika hali ya kubadilisha katiba zao ili ziiendane na demokrasia magharibi.

katika michakato ya katiba kuna vitu vingi vinavyotokea mfano wananchi kutoa maoni yao, kupitia katiba ya zamani,  kuangalia katiba za watu wengine n.k.

tukumbuke kuwa rasimu yetu ya katiba imechukua baadhi ya vifungu kutokanan na maoni yetu na vingine kutoka katiba na rasimu za wezentu hasa ile ya kenya ya 2010 ambayo ndiyo imesimamia  uchaguzi wa Kenya ulioisha.

katiba yetu ya mwaka 1977, ilikuwa haina kifungu kinacho ruhusu matokeo ya uraisi kuhojiwa mahakamani baada ya kutangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi. jambo hili lililamikiwa kwa muda mrefu n wanaharakati na hatimaye rasimu hii ya 2013 imeweka kifungu kinacho ruhusu hilo.

lakini mbali na kuweka kifungu hicho bado kina mapungufu y kimsingi yanyokifanya kifungu chenyewe kutokuwa na maana. kwani kinatoa haki upande mmoja na kinany'anganya  haki upande mwingine. kifungu hiki bali na maoni ya wannchi, msingi wake mkubwa ni rasimu ya kenya ya mwaka 2010. yenye kifungu kama hicho.
ukisoma rasmu ibara ya 78 (1) inasomeka hivi "kwa kuzingatia masharti ya ibara ndogo ya (2), endapo mtu yeyote aliyeshiriki kama mgombea nafasi ya madaraka ya Rais katika uchaguzi wa Rais hakuridhika na matokeo ya uchaguzi huo anaweza kuwasilisha malalamiko katika Mahakama ya juu kupinga matokeo ya Rais yaliyotangazwa na tume huru ya uchaguzi."

              (2) malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais yatawasilishwa mahakama ya juu ndani ya muda wa siku saba baada ya siku ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa Rais.

79 (1)Rais mteule ataapishwa na Jaji mkuu na atashika nafasi ya madaraka ya Rais mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote hatashika madaraka kabla ya kupita siku thelathini kutoka siku matokeo ya uchaguzi wa Rais yalipotangazwa na Tume Huru  ya Uchaguzi au siku ya kuthibitishwa na  Mahakama ya Juu.

ukisoma vizuri vifungu hivi utaona kabisa kimoja kinauliwa na kingine na hasa cha 78 hakina nguvu yeyote dhidi ya kifungu cha 79, kwani hakijatoa muda kwa watu au mtu mwenye lalamiko juu ya matokeo. raisi akishaapa tiyari atakuwa ameshika madaraka na kuwa raisi pia. 

na kama tutaacha kifungu cha 79 kiendelee kusomeka kama kilivyo basi tutategemea sana busara za viongozi wa tume ya uchaguzi. 

kifungu hiki tume kitoa kenya na katiba ya kenya inaonyesha vizuri na imeweka siku za kuapishwa sio kutangazwa na kuaapa.

soma  kifungu cha 140 na 141 cha katiba ya kenya hapo chini.
 
 Ibara ya 140. Maswali kama uhalali wa uchaguzi wa rais

(1) Mtu anaweza kuwasilisha malalamiko katika Mahakama Kuu kupinga uchaguzi wa Rais mteule ndani ya   siku saba baada ya tarehe ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi wa rais.
(2) Ndani ya siku kumi na nne baada ya kufungua jalada la malalamiko hayo chini ya kifungu cha (1), Mahakama Kuu itasikiliza na kuamua malalamiko na uamuzi wake utakuwa wa mwisho.
(3) Kama Mahakama Kuu huamua uchaguzi wa Rais mteule kuwa batili, uchaguzi mpya utafanyika ndani ya siku sitini baada ya uamuzi.

Ibara ya 141. Kushika madaraka ya Rais
(1) kuapishwa kwa Rais mteule-watakuwa katika umma mbele ya Jaji Mkuu, au, kutokana na kukosekana kwa Jaji Mkuu, Naibu Mkuu wa Sheria.
(2) Rais mteule-ataapishwa juu ya yafuatayo kwanza Jumanne -
        (A) siku ya kumi na nne baada ya tarehe ya tangazo la matokeo ya uchaguzi wa rais, kama hakuna malalamiko imekuwa filed chini ya Ibara ya 140; au
        (B) siku ya saba baada ya tarehe ambayo mahakama mithili uamuzi kutangaza uchaguzi kuwa halali,       ikiwa dua yoyote imekuwa filed chini ya Ibara ya 140.
(3) Rais mteule kushika madaraka kwa kuchukua na subscribing kiapo au uthibitisho wa utii, na kiapo au tamko la dhati kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi, kama ilivyoainishwa katika Jedwali la Tatu.
(4) Bunge na sheria kutoa kwa ajili ya utaratibu na sherehe kwa ajili ya kuapishwa kwa Rais mteule.

ndugu zangu naomba mlinganishe vifungu hivi. 

Thursday, 15 August 2013

MAMBO YA AMANI NA USALAMA WA TAIFA


Kuna mambo mabayao kimsiungi sikutaka kuyajadli ila nataka kuyajadili hii jioni, lakini kwa kuwa tiyari yameanza kujitokeza ni lazima niyaseme. hapa nchini tumekuwa na matatizo ya amani na usalama. na mambo haya yako katika ngazi ya taifa na kimataifa.

Hatari kwa taifa  (national threat) ni jambo ambalo laweza kuanzia ndani ya nchi au nje ya nchi , na ni wajibu wa nchi husika kujua kuwa iko katika hali ya hatari. hatari ya kutoka ndani inaweza kuundwa katika mazingira ya aina mbili moja inaweza kuundwa na vikundi vya waasi au wananchi wachache tu, na msingi  mkubwa wa vikundi hivi huwa kwa mara nyingi ni kutoridhika na matendo ya serikali au kikundi cha watu ndani ya serikali.
Wakati mwingine suala hili linaweza kuchochewa na serikali yenyewe bila kujua au kwa kujua. mfano serikali inaweza kuwabagua watu fulani kwa tofauti zao za kisiasa, kikabila , kiuchumi, kiimani na kikabila na kuwalazimisha kuunda kikundi. Kukiibuka kikundi kilichochowe na serikali basi hicho inakuwa ni vigumu mno kikigundua kwa sababu kinakuwa kinapigana na kikundi kingine bila kukilenga moja kwa moja. mfano mzuri ni vita ya Kongo au Biafra ya Naigeria ambapo serikali ilichochea tofauti za kidini kuanzia enzi za mkoloni na ikaja kuwa vita dhidi ya uislamu na ukristo lakini kupitia serikali.

wakati mwingine serikali inaweza kusababisha hili kwa kufanya ugaidi kwa watu wake mfano kuwateka na kuwapiga kuwaumiza, na katika mazingira kama haya serikali huwa inatumia sura ya kulinda amani na kuwalinda raia anowapiga. Hili limeanza kutokea hapa nchini. mtakumbuka kuwa bado kuna mvutano wa polisi na wanaharakati kuhusu suala la Daudi Mwangosi, Ndugu Absalom Kibanda, Dr Ulimboka, na sasa  Ndugu Ponda na mengine mengi.

Upande mwingine hatari ya taifa inaweza kutoka mataifa jirani na mengine ya nje. Taifa linaweza kuwa na marafiki ambao kimsingi wanaweza kuwa hatari kwa upande mwingine kulingana na mtandao wa itikadi na maslahi ya kiuchumi na kisiasa. mtakumbuka  suala la vita dhidi ya Ethiopia na Eriteria ambapo Amerika alijenga uadui na Misiri baada ya kusemekana kushirikiana na Israel kumsaidia Ethiopia dhidi ya Eritria.

lakini tusisahahu pia kuwa hata taifa husika linaweza kusababisha hatari kutoka nje, hali hii inaweza kutokea kupitia matamshi ya viongozi wakuu na wasimamizi wa serikali dhidi ya matifa mengine, au vyombo vya habari , mazoezi ya kijeshi mipakani n.k
 kwa hatua hii ebu nieleze suala hili kidogo kuhusu tanzania. hapa nchini kumekuwapo kumbukumbu nzuri ya watu kuvamiwa na kutekwa kunyanyaswa na pengine na watu wasio julikana lakini yakitokea hayo unasikia marumbano kati ya vyombo vya dola na makundi ya wanaharakti na wansiasa. lakini mbali na kuvutana huko hakuna siku umma wa Watanzania umeambiwa ukweli ni huu. tunabaki kujivicha kwenye ugaidi, udini na siasa tu.
leo niliposoma gazeti moja hapa nchini niliona likitaja kifo cah Prof Mwakusa ambaye alipigwa risasi muda mrefu kidogo na wanfunzi wa chuo kikuu na vyuo rafiki nchini waliaaandamanan wakitaka uchunguzi wa wauaji hao lakini mpaka sasa hakuna jibu. na kumbuka wakti huu nilikuwa mwanfunzi katika chuo hicho hivyo maneno yote yaliyo kuwa yanzungumzwa nilikuwa nayasikia na kuyaona.

lakini tunakumbuka kupigwa risaiasi kwa mwandishi wa habari Daudi Mwangosi, akiwa katika  shughuli zake za habari. Suala hili limeishia kukamtwa kwa kijana polisi mdogo na kufunguliwa mashitaka ya kumpiga risasi lakini ukiangalia mwennendo wa kesi unapata wasiwasi. ni sababu gani ya mtuhumiwa wa mauaji analindwa na serikali tena kwa kupigiwa ving'ora wakti akipelewkwa mahakamni na pengine kufungiwa misafara mirefu ya magari ya serikali hali kama hii inatia wasiwasi machoni pa watnzania.

tukio jingine nilile la kijana aliyepigwa risasi katika mkutano wa CHADEMA pale Morogoro. Serikali kupitia jeshi la polisi wakatwambia amepigwa na kitu kizito. lakini naye hatuoni kesi juu ya hilo. hatu uchunguzi wa jambo hilo haujawekwa wazi hata siku moja.
 lakini kuna kutekwa kwa DR Ulimboka  na kupigwa kwa Mwandishi wa habari  Absalom kibanda. matukio yote haya tunasikia mivutano ya polisi na wansiasa na pengine kutupa vichwa vy habari katika magazeti. je wananchi tufikiriea nini juu ya haya mabo.?
 tukiachia hayo tunakumbuka mabomu ya Mbagara na Gogo la Mboto hakuna taarifa tumepata, mabomu yaliyopigwa Arusha na baada kutumia nguvu za polisi kutumika katika mazishi ya waanga wa tukio hilo.
lakini ukiangalia matamshi ya viongozi wetu utaona kabisa kuna hatari mfano sio muda mrefu tulimsikia waziri mkuu kaiwatangazia polisi na vyombo vya usalkama kuwa " wapigeni tu"
sasa mambo kama haya yanatupa wasiwasi wananchi wakawaida.